Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Viongozi, Wanachama CCWT wazidi kuvutana
Habari Mchanganyiko

Viongozi, Wanachama CCWT wazidi kuvutana

Katibu wa Chama cha Wafugaji nchini, Magambe Makoye (katikati) akionesha nyaraka kwa waandishi wa habari
Spread the love

BAADHI ya wajumbe na wanachama wa Chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT) wameendelea kuvutana na uongozi wa juu chama hicho wakitaka viongozi kuachia madaraka na kufanyika uchaguzi, anaandika Dany Tibason.

Baadhi ya madai ya wanachama na wajumbe wa chama hicho kutaka viongozi kuachia ngazi ni pamoja na kudaiwa kushindwa  kutimiza majukumu yao ikiwa ni pamoja na kushindwa kuitisha mkutano wa kusoma mapato na matumizi.

Hoja nyingine ni pamoja na kudai kwamba viongozi hao wanafanya ujanja wa kubadili kadi za uanachama wa chama hicho ikiwa ni pamoja na kubadili nembo ya awali ya chama hicho.

Mmoja wa Wenyeviti hao,Wamarwa Kusundwa alisema kuwa waliuchagua uongozi wa mpito ambao ni mwenyekiti, katibu mkuu, mtunza hazina pamoja na wajumbe 12 wa kamati tendaji mnamo mwaka 2015 kwa lengo la kutetea maslahi ya wafugaji.

“Kwa kweli tunashindwa kuuelewa uongozi huu wa sasa kwa sababu umekuwa ukijifanyia mambo kivyake bila kushirikisha kamati tendaji wala bodi ya wadhamini na mbaya zaidi hawajawahi kusoma mapato na matumizi tangu wachaguliwe,”alisema.

Katibu wa Chama cha Wafugaji nchini, Magambe Makoye hakuwa tayari kuzungumzia sakata hilo alipotakiwa kutoa ufafanuzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

error: Content is protected !!