JESHI la Polisi mkoani Arusha linawasaka viongozi wa kijiji cha Kisimiri Juu kilichopo wilayani Arumeru kwa tuhuma za kukiuka agizo la serikali pamoja na kukwamisha msako wa bhangi kijijini hapo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Hayo yalisemwa jana tarehe 27 Septemba 2018 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng’azi wakati kizungumza na Wanahabari mkoani humo.
Kamanda Ng’azi alisema kuwa, viongozi hao walifunga ofisi huku wanakijiji wakijificha wakati wa msako uliofanyika alfajiri ya jana baada ya Jeshi la Polisi kudokezwa kuhusu usafirishaji wa bangi uliopangwa kufanyika jana.
“Tunaendelea kuwatafuta viongozi wa kamati za ulinzi na usalama na wa kijiji, kwa ajili ya kuwachukulia hatua za kisheria kwa kuwa wana wajibu wa kuhakikisha katika eneo lao hakuna biashara ya dawa za kulevya inayofanyika.
“Viongozi hao wamekiuka agizo la serikali linalomtaka kila kiongozi katika eneo lake ahakikishe kwamba halilimwi bhangi,” alisema Kamanda Ng’azi.
Leave a comment