Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Viongozi wa mashitaka Uganda wasitisha mgomo
Kimataifa

Viongozi wa mashitaka Uganda wasitisha mgomo

Yoweri Museven, Rais wa Uganda
Spread the love

VIONGOZI wa mashitaka nchini Uganda waliogoma wakidai  ongezeko la mishahara wamekubali ombi la serikali la kurejea kazini huku wakati madai yao yakishughulikiwa, anaandika Catherine Kayombo.

Serikali iliwaomba viongozi hao miezi mitatu kushughulikia madai yao, na kuwaomba kurejea kazini ili kuepusha msongamano wa kesi nchini humo ingawa ombi hilo lilikataliwa awali.

Msemaji Mkuu wa muungano wa viongozi wa mashtaka, Awali Kizito, aliiwaambia wanahabari kuwa mkutano mkuu ndiyo utakaoamua kusitisha ama kuendelea na mgomo huo.

“Hatima ya mgomo wetu ipo mikononi mwa mkutano mkuu wa wanachama wetu, tunatarajia kukutana  na kuamua ikiwa tutakubali ombi la serikali kusitisha mgomo huu au la”, alisema Kizito.

Viongozi hao  waliokuwa wamegoma kwa takribani wiki moja,  walikutana jana kuamua endapo wasitishe mgomo huo ambao umekwamisha kesi mahakamani.

Kufuatia mgomo huo, majaji wamekuwa wakiahirisha na kuchelewesha  kesi kwa ukosefu wa waendesha mashtaka.

Moja ya kesi zilizocheleweshwa nchini humo ni ya mauaji ya aliyekuwa msemaji wa polisi, Andrew Felix Kaweso.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!