Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Viongozi wa dini kupambana na Saratani Mlango wa Kizazi
Afya

Viongozi wa dini kupambana na Saratani Mlango wa Kizazi

Dk. Faustin Ndungulile
Spread the love

VIONGOZI wa dini kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamie, Jinsia, Wazee na Watoto wanakusudia kufanya kongamano la pamoja kujadili uanzishwaji wa chanjo ya kukinga Saratani ya Mlango wa Kizazi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mkurugenzi wa maandalizi ya maombi hayo ya kitaifa yatayofanyika jijini Dodoma kuanzia 22 hadi 30 Juni mwaka huu, Askofu Mkuu wa Kanisa la Endtime Haverst Tanzania Dk. Elia Mauza amesema, maandalizi hayo yamefikia asilimia 100.

Aidha Dk. Mauza ambaye pia ni Kaimu Mratibu wa Engenger Health amesema kuwa, viongozi wa dini kwa kushirikiana na wadau wa afya, wanalenga kuhakikisha wanashirikiana ili kutatua matatizo ya afya.

Amesema kuwa, wizara hiyo kwa kushirimiana na wadau wa Engenger Health, wameandaa kikao maalum cha kuongea na viongozi wa dini pamoja na waandishi wa habari ili kujadili masuala ya chanjo hususani chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi.

Dk. Mauza amesema, wizara kupitia mpango wa Taifa imepanga kufanya kikao hicho kesho tarehe 16 Mei 2019 katika ukumbi wa mikutano katika Hotel ya Morena, Jijini Dodoma.

Amesema, lengo la kikao hicho ni kujadili mafanikio na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa huduma ya chanjo ya kukinga mabinti dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi tangu ianzishwe Aprili mwaka jana.

“Baada ya kuanzishwa chanjo hii mwitikio ulikuwa ni mkubwa,lakini baada ya kuanzishwa kumekuwa na kiwango cha chini kwa dozi ya pili” amesema Dk. Mauza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!