Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Viongozi ACT-Wazalendo mbaroni kwa kufungua matawi bila kibali
Habari za SiasaTangulizi

Viongozi ACT-Wazalendo mbaroni kwa kufungua matawi bila kibali

Ado Shaibu, Katibu Mkuu ACT-Wazalendo
Spread the love

ADO Shaibu, Katibu wa Itikadi na Uenezi   wa Chama cha ACT Wazalendo, na viongozi wa chama hicho Mkoa wa Dar es Salaam, wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kufungua matawi bila kibali. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 14 Septemba 2019 na Salim  Bimani, Mwenyekiti wa Kamati ya Itikadi, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma ACT-Wazaleno.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bimani, viongozi hao wamekamatwa leo wakati wanafungua matawi mapya ya ACT-Wazaleno kwenye Kata ya Azimio, Jimbo la Temeke jijini Dar es Salaam.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, Ado pamoja na Soud Salum, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Mkoa wa Dar es Salaam, Risasi Semasaba Katibu wa Uchaguzi wa mkoa huo na Katibu wa Ngome ya Vijana wa Kata ya Azimio, Said wamepelekwa katika Kituo cha Polisi Chang’ombe.

“Polisi wanadai kushikiliwa kwa viongozi hao ni kukosa kibali cha ufunguaji wa matawi hayo. Viongozi hao wamepelekwa kituo cha Polisi Chang’ombe kwa mahojiano.

Chama cha ACT Wazalendo tunalaani kitendo hicho cha Jeshi la Polisi kuingilia masuala ya vyama vya Siasa na kuvizuia kutekeleza wajibu wao wa kisheria,” inaeleza taarifa ya Bimani.

Bimani ametoa wito kwa Jeshi la Polisi kuwaacha huru wanasiasa hao sambamba na kusimamia wajibu kwa kukwepa kuvikandamiza vyama vya siasa vya upinzani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!