RAIS wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa na Imran Khan, Waziri Mkuu ni miongoni mwa viongozi 140 waliosaini barua kwenda Shirika la Afya Duniani (WHO), wakishauri dawa ya corona itakapopatikana, igawiwe bure kwa watu wote. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Wamesema, dawa pamoja na chanjo yake inapaswa kugawiwa bure, na iwe haki ya kila mwanadamu kupata dawa hiyo ili aishi.
“Dawa ya corona haipaswi kuwa biashara duniani, wanasayansi watakaovumbua wawaeleze wanasayansi wenzao namna ya utengeneza.”
“Serikali za mataifa lazima ziungane duniani kote ili kuhakikisha kwamba, pale dawa itapopatikana, inazalishwa kwa wingi na haraka na zinasambazwa kwa watu wote, katika mataifa yote bila malipo,” barua hiyo imeeleza, na kuongeza:
“Tiba, utambuzi na uvumbuzi wowote ulio na uhusiano na CIVID-19, unapaswa kuelezwa kwa mataifa yote bila ubaguzi.”
Pia, Rais Ramaphosa jana jioni Jumatano tarehe 13 Mei 2020, alipohutubia taifa hilo alisema, nchi yake licha ya maambukizi kufika 12,000, bado mpango wa kuondoa vikwazo vya kukaa ndani unaendelea na anatarajia mwishoni mwa mwezi huu, watu wataendelea na shughuli zao kama kawaida.
Ramaphosa alisema, “baadhi ya maeneo yaliyoathiriwa zaidi na COVID-19 nchini humo yataendelea na utaratibu wa kujifungia mpaka maambukizi yatakapopungua.”
Mpaka tarehe ya leo, Afrika Kusini imeshuhudia vifo 219 vilivyotokana na ugonjwa wa corona.
Leave a comment