Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Vijana wa Burundi ”wazamia” nchini Marekani
Kimataifa

Vijana wa Burundi ”wazamia” nchini Marekani

Pierre Nkurunziza, Rais wa Burundi
Spread the love

VIJANA sita wakiwamo wavulana wanne na wasichana wawili kutoka  Burundi waliokuwa wakishiriki katika mashindano ya roboti yaliyokuwa yakifanyika  jijini Washington DC, wametoweka nchini Marekani na haijulikani walipo hadi sasa,  anaandika Catherine Kayombo.

Waliotoweka nchini Marekani ni  Don Ingabire, Kevin Sambukiza,Nice Munezero, Audry Mwamikazi, Richard Irakoze na Aristide Irambona.

Waandaaji wa mashindano hayo ya kwanza duniani wamesema kuwa wametoa taarifa polisi baada ya msimamizi wa timu hiyo ya Burundi kushindwa kuwapata vijana hao.

Msemaji mkuu katika mashindani hayo, Jose Escotto amesema ripoti kuu imeshawasilishwa kwa polisi na wako wanachunguza kupotea kwa vijana hao.

Idara ya polisi jijini Washington, imesema kuwa vijana hao walionekana kwa mara ya mwisho siku ya jumanne wakati wa kufunga michezo hiyo.

Imebandika picha za vijana hao katika mtandao wa twitter na kuwataka raia kuwasiliana nao endapo watawaona vijana hao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!