Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Vigogo wawili wasakwa kwa ununuzi haramu wa dhahabu
Habari Mchanganyiko

Vigogo wawili wasakwa kwa ununuzi haramu wa dhahabu

Madini ya dhahabu
Spread the love

NAIBU Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo ameagiza Jeshi la Polisi kuwakamata wafanyabiashara Mansoor Almasi na Jacob Mwapinga wanaotuhumiwa kufanya ununuzi haramu wa madini ya dhahabu kwenye Mgodi wa Ulata ulioko mkoani Iringa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Nyongo ametoa agizo hilo baada ya wafanyabaishara hao kukaidi wito wake pamoja na kuonana na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela.

Katika hatua nyingine, Nyongo ameagiza jeshi la polisi kuwakamata wamiliki wa mgodi wa dhahabu wa Nyakavangala, kufuatia wamiliki hao kuwasilisha kwake taarifa isiyo sahihi kuhusu namna ya mgodi huo unavyoendeshwa,  ulipaji kodi na mrabaha wa serikali.

Nyongo yuko ziarani mkoani Iringa, ambapo katika ziara yake alizungumza na wachimgaji wadogo na mmiliki wa mgodi wa Ulata, Ibrahimu Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!