Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Vigogo wamiminika bungeni, JPM kulifunga Bunge
Habari za Siasa

Vigogo wamiminika bungeni, JPM kulifunga Bunge

Marais Wastaafu wa Tanzania
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Magufuli leo Jumanne tarehe 16 Juni 2020 analihutubia Bunge la 11 na kulivunja jijini Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea),

Bunge hilo la 11 linaloongozwa na Spika Job Ndugai lilizinduliwa na Rais Magufuli tarehe 20 Novemba 2015.

Tayari wageni mbalimbali wa Kitaifa na Kimataifa wamekwisha kuwasili ukumbini kumsubiri Rais Magufuli kuingia ndani ya ukumbi huo.

Baadhi ya wageni hao ni; Marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete.

Pia, Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar, Mohamed Ali Shein, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Ali Seif Iddi, Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma na Makamu wa Rais mstaafu wa Tanzania, Mohamed Gharib Bilal.

Kulifunga Bunge hilo, kunatoa fursa ya mchakato wa uchaguzi mkuuutakaofanyika Oktoba 2020 kuanza.

Wengine waliopo ni, mawaziri wakuu wastaafu, Frederick Sumaye, Mizengo Pinda na Edward Lowassa.

Pia, Spika Mstaafu Anne Makinda, Jaji Mkuu mstaafu, Othuman Chande, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama ni miongoni mwa waliojitokeza katika shughuli hiyo ya kihistoria.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE & MwanaHALISI  TV kwa habari zaidi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!