Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Vigogo wa CCM wasakwa kwa ulawiti, ubakaji
Habari za SiasaTangulizi

Vigogo wa CCM wasakwa kwa ulawiti, ubakaji

Pingu
Spread the love

KATIBU Mwenezi wa CCM Kata ya Mkolani, Zephilin Michael na Katibu Mwenezi wa chama hicho katika kata ya Buhongwa, Hassan Bushangama wanasakwa na Jeshi la Polisi mkoani Mwanza kwa tuhuma za ubakaji na ulawiti. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa ya Jeshi la Polisi mkoani Mwanza liyotolewa leo tarehe 31 Oktoba 2018 na Kamanda wa Polisi mkoani humo, Jonathan Shanna inaeleza kuwa, Mtuhumiwa wa kwanza ambaye ni Michael anadaiwa kutenda kosa la ulawiti dhidi ya kijana wake wa kazi tarehe 26 Oktoba 2018.

Michael anadaiwa kumpangishia kijana huyo mwenye umri wa miaka 16 chumba katika nyumba ya wageni iliyopo katika Kata ya Mkolani, eneo ambalo alilotumia kumfanyia ukatili huo, kisha kutoroka baada ya kijana kupiga kelele za kuomba msaada kutoka kwa raia wema.

Taarifa hiyo ianeleza kuwa, mtuhumiwa wa pili ambaye ni Bushangama anadaiwa kumbaka na kumpatia ujauzito mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17, wa kidato cha pili katika shule ya Sekondari Buhongwa.

Bushangama anasakwa na Jeshi la Polisi baada ya kutoroka wakati polisi wakiendelea na taratibu za kumfikisha mahakamani.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, Jeshi la Polisi linawashikilia watu wawili,Jafari Swalehe na Mgassa Carlos wanaodaiwa kumtorosha mtuhumiwa huyo, ambao awali walikuwa ni wadhamini wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!