KATIBU Mwenezi wa CCM Kata ya Mkolani, Zephilin Michael na Katibu Mwenezi wa chama hicho katika kata ya Buhongwa, Hassan Bushangama wanasakwa na Jeshi la Polisi mkoani Mwanza kwa tuhuma za ubakaji na ulawiti. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Taarifa ya Jeshi la Polisi mkoani Mwanza liyotolewa leo tarehe 31 Oktoba 2018 na Kamanda wa Polisi mkoani humo, Jonathan Shanna inaeleza kuwa, Mtuhumiwa wa kwanza ambaye ni Michael anadaiwa kutenda kosa la ulawiti dhidi ya kijana wake wa kazi tarehe 26 Oktoba 2018.
Michael anadaiwa kumpangishia kijana huyo mwenye umri wa miaka 16 chumba katika nyumba ya wageni iliyopo katika Kata ya Mkolani, eneo ambalo alilotumia kumfanyia ukatili huo, kisha kutoroka baada ya kijana kupiga kelele za kuomba msaada kutoka kwa raia wema.
Taarifa hiyo ianeleza kuwa, mtuhumiwa wa pili ambaye ni Bushangama anadaiwa kumbaka na kumpatia ujauzito mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17, wa kidato cha pili katika shule ya Sekondari Buhongwa.
Bushangama anasakwa na Jeshi la Polisi baada ya kutoroka wakati polisi wakiendelea na taratibu za kumfikisha mahakamani.
Taarifa hiyo inaeleza kuwa, Jeshi la Polisi linawashikilia watu wawili,Jafari Swalehe na Mgassa Carlos wanaodaiwa kumtorosha mtuhumiwa huyo, ambao awali walikuwa ni wadhamini wake.
Leave a comment