Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Vigogo kampuni ya vinywaji kortini tuhuma za utakatishaji Bil.1.6
Habari Mchanganyiko

Vigogo kampuni ya vinywaji kortini tuhuma za utakatishaji Bil.1.6

Melanie Phillippe na Ntemi Massanja wakiwa Mahakama ya Kisutu, Dar es Salaam
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) nchini Tanzania, imewafikisha Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam watuhumiwa watatu kati ya wanne waajiriwa wa Kampuni ya BEVCO LTD kwa tuhuma za rushwa na utakatishaji fedha zaidi ya Sh.1.6 bilioni. Anaripoti Mwandishi Wetu.

Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi tarehe 19 Novemba 2020 na Afisa Habari wa Takukuru, Doreen Kapwani imesema, watuhumiwa hao wa kampuni hiyo inayojihusisha na uagizaji na uuzaji wa vinywaji vikali kutoka nje, wawili ni raia wa Tanzania na wengine wa Ufaransa.

Doreen amesema, uchunguzi wa awali uliofanywa na Takukuru umebaini, kampuni hiyo ambayo imesajiliwa Tanzania kwa ajili ya biashara hiyo tangu mwaka 2017, katika kutekeleza shughuli zake za biashara, wamekuwa wakichepusha Kodi ya Ongezeko laThamani (VAT) ambayo ilipaswa kulipwa serikalini.

Melanie Phillippe na Ntemi Massanja wakiwa Mahakama ya Kisutu, Dar es Salaam

Amesema, vitendo hivyo vya kihalifu, watuhumiwa wote wanne walikwepa kodi ya Sh.1.65 bilion na kuzitakatisha.

Amewataja watuhumiwa hao ni; Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Thiery Lefuevre na Meneja Rasilimali Watu, Melanie Phillippe ambao wote ni raia wa Ufaransa.

Mwingine ni, Ntemi Massanja, Mwanasheria wa BEVCO kutoka Kampuni ya Gabriel & Company Anttornys-AT Law huku Joseph Rwegasira Samson akiendelea kutafutwa.

“Atakayefanikisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyu, atapewa donge nono la Sh.10 milioni,” amesema Doreen

Ametaja makosa ambayo wanatuhumiwa nayo ni; kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo kwa mamlaka, kula njama ya kutenda kosa la uhujumu uchumi, kushindwa kulipa kodi ya ongezeko la thamani, kuisababishia serikali hasara na kutakatisha fedha.

1 Comment

  • Uchaguzi wa mwaka huu jinsi ulivoendeshwa itakuwa ndo mwisho watu kupiga kula la sivyo tume mpya iuundwe.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!