Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Halima Mdee achomoka mahabusu
Habari za SiasaTangulizi

Halima Mdee achomoka mahabusu

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe
Spread the love

HALIMA Mdee, Mbunge wa upinzani katika jimbo la Kawe, jijini Dar es Salaam amepata dhamana leo baada kukaa ndani kwa saa 24. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI ONLINE, wakili wa Mdee, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema, Hekima Mwasipu amesema, Mdee kwa sasa yupo huru.

“Baada ya kuhangaika toka jana sasa tumepata dhamana, ataripoti tarehe 26 mwezi huu,” amesema.

Mdee alishikiliwa na jeshi la polisi jana tarehe 23 Februari 2019 kwa tuhuma ya kutoa kauli za kashfa dhidi ya Rais wa Jamhuri, Dk. John Pombe Magufuli.

Mdee anadaiwa kutoa kauli ya uchochezi alipokuwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Kata ya Mikocheni, tarehe 21 Februari 2019.

Amedaiwa kusema “mtu ananunua ndege badala ya vifaa vya zahanati, hii ni akili au matope.”

Awali Wakili Mwasipu alisema “Mdee alipokea wito wa kutakiwa kufika kwenye ofisi ya mkuu wa upelelezi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni (RCO). Alitekeleza agizo hili. Alifika kituoni hapo saa 3 asubuhi.”

Hata hivyo, baada ya kuitikia wito, aliendelea kushikiliwa na polisi mpaka alipopata dhamana leo.

Mwasipu amesema, utaratibu hauruhusu mtuhumiwa kukaa mahabusu zaidi ya saa 24 “ni haki ya Mdee kupata dhamana.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!