Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Vigogo Acacia wasomewa mashtaka 39
Habari Mchanganyiko

Vigogo Acacia wasomewa mashtaka 39

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

VIGOGO katika kampuni ya madini ya Acacia, akiwemo aliyekuwa Makamu wa Rais, Deo Mwanyika na Mshauri wa Serikali ndani ya kampuni hiyo, Alex Lugendo leo tarehe 17 Oktoba 2018 wamepandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka 39. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mwanyika na Lugendo wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mfawidhi, Kelvin Mhina na kusomewa mashtaka yanayowakabili ikiwemo ya kughushi na kula njama pamoja na utakatishaji fedha, huku wengine wanne wakitarajiwa kufikishwa kizimbani hivi karibuni.

Watuhumiwa hao wanadaiwa kufanya makosa hayo katika nyakati tofauti, ambapo katika shtaka la kwanza la kula njama, wanadaiwa kulifanya mwezi Juni na Novemba mwaka 2008 ndani ya nchi na nje ya nchi.

Mwanyika na Lugendo walisomewa mashtaka yao na Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi akisaidiana na Shadrack Kimoro na Jacqline Nyantole.

Kabla ya kupandishwa kizimbani, watuhumiwa hao walikamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) tangu juzi tarehe 15 Oktoba 2018, ambapo taarifa ya taasisi hiyo ilitaja sababu za kuwakamata kuwa ni pamoja na matumizi mabaya ya ofisi kwenye tasnia ya madini.

Taarifa ya TAKUKURU ilidai kuwa, watuhumiwa hao walishindwa kusimamia nchi kupata mapato kama ilivyotarajiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!