Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Video ya ngono ya Waziri yavuja, aomba radhi
Kimataifa

Video ya ngono ya Waziri yavuja, aomba radhi

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Afrika Kusini, Malusi Gigaba
Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani wa Afrika Kusini, Malusi Gigaba yuko katika wakati mgumu baada ya video ya ngono iliyomhusisha yeye na mkewe kuvuja mitandaoni. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Katika utetezi wake kupitia akaunti yake ya Twitter, jana aliandika kuwa, video hiyo imevujishwa na wahalifu wa mtandaoni walio ingilia simu yake, huku akidai kwamba ni miongoni mwa mashambulizi ya kisiasa yaliyoanza kuibuka tangu alipoteuliwa kuwa Waziri wa Fedha Machi 31, 2017.

Gigaba amejitetea kuwa, alijirekodi video hiyo kwa ajili ya matumizi yake binafsi lakini imesambazwa na wahalifu baada ya mawasiliano yake kuingiliwa.

“Mke wangu na mimi tumejifunza, tumejutia na kuhuzunika kuona kwamba video ya ngono ambayo ilikuwa kwa ajili ya macho yetu imeibiwa wakati mawasiliano yangu yameingiliwa. Nachukua fursa hii kuomba msamaha kwa umma na familia yangu hasa watoto wangu, mama yangu, mkwe wangu kwa maumivu na aibu kufuatia video hii iliyosambazwa mitandaoni,” aliandika Gigaba Twitter.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!