Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Uteuzi wa Rais Magufuli leo hii
Habari Mchanganyiko

Uteuzi wa Rais Magufuli leo hii

Dk. John Magufuli, Rais wa Tanzania
Spread the love

RAIS John Magufuli amemteua Dk. Michael Ng’umbi kuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW).Anaripoti Bupe Mwakiteleko…(endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo tarehe 20 Februari 2019 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa.

Taarifa hiyo ya Msigwa inaeleza kuwa, Dk. Ng’umbi amechukua nafasi ya Dk. Fidelice Mafumiko ambaye ameteuliwa kuwa Mkemia Mkuu wa Serikali.

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Ng’umbi alikuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Kitivo cha Elimu cha Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT).

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amemteua Jaji Stephen Magoiga kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani (FCT). Kabla ya uteuzi wa Jaji Magoiga, nafasi hiyo ilikuwa chini ya Jaji Barke Mbaraka Sehel ambaye ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.

“Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa viongozi huo umeanza tarehe 19 Februari 2019,” inaeleza sehemu ya taarifa ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!