Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Utafiti rushwa ya ngono: Watumishi 68.6% wakiri
Tangulizi

Utafiti rushwa ya ngono: Watumishi 68.6% wakiri

Spread the love

UTAFITI  wa rushwa ya ngono katika taasisi za elimu ya juu uliohusisha vyuo vikuu viwili vya  Dar es Salaam na Dodoma, umewasilishwa leo tarehe 4 Disemba 2020, jijini Dodoma. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mtafiti wa rushwa ya ngono nchini, Dk. Juvinary John amesema katika utafiti huo, jumla ya watu 589 walihojiwa juu ya uelewa wa rushwa ya ngono. 

Ameanisha makundi yaliyohojiwa kuwa wanafunzi asilimia 81.6, watumishi asilimia 91.4 walieleza uwepo wa rushwa ya ngono Katika taasisi za elimu ya juu.

Kuhusu uwepo wa rushwa ya ngono, watumishi asilimia 68.6 walisema ‘ndio,’ watumishi asilimia 31.4 walisema ‘hapana,’ wanafunzi asilimia 57.5 walisema ‘ndio’ huku wanafunzi asilimia 42.5 walisema ‘hapana.’

Aidha, ameeleza  sababu za kuwepo kwa rushwa ya ngono kuwa, kundi la wanafunzi mwitikio wao walisema ni pamoja na ukosefu wa maadili asilimia 63, ushawishi wa mtu mwenye mamlaka asilimia 27.7, mfumo wa utoaji taarifa kutokuwa rafiki asilimia 9.3.

Amebainisha mbinu zinazotumika kwenye rushwa ya ngono katika  elimu ya juu ni pamoja na kutoa alama za chini na vitisho vya kutofaulu.

Ofisa Uhusiano kutoka taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini Doreen Mapwani pamoja na mkurugenzi wa uzuiaji rushwa wa Taasisi hiyo, Sabina Seja wamesema, taasisi hiyo inaendelea kutoa ushirikiano katika mapambano dhidi ya rushwa hususan rushwa ya ngono.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma, Dk. Ombeni Msuya amesema, chuo kimeimarisha kamati zote kwa kusimamia madaraja ya jinsia ambapo kuna masanduku 106 ya kutoa maoni juu ya changamoto.

Naye Mkurugenzi wa Taaluma na Jinsia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. Lulu Mahan amesema, chuo hicho kimekuwa kikitoa adhabu kwa watumishi wanaobainika kujihusisha na rushwa ya ngono ikiwa ni pamoja na kuwafukuza.

Mkakati wa utafiti wa kupambana na rushwa ya ngono ulianza tarehe 18 Juni 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!