Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Urais Z’bar: Rais Magufuli atoa onyo kali wagombea 31, asema…
Habari za SiasaTangulizi

Urais Z’bar: Rais Magufuli atoa onyo kali wagombea 31, asema…

Rais John Magufuli, Mwenyekiti wa CCM, akizungumza mara baada ya kurudisha fomu ya kuwania Urais kwa tiketi ya CCM
Spread the love

RAIS John Magufuli, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), ameonya wanachama wa chama hicho waliojitokeza kuwania urais Zanzibar kutochafuana na kuhakikisha wanaheshimiana na kuzingatia taratibu za chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Amesema, kazi si moja ya urais pekee bali kuna nafasi zingine ndani ya Serikali za uteuzi hivyo si lazima kuanza kuchafuana ikiwemo kupitia mitandaoni.

Rais Magufuli ametoa onyo hilo leo Jumanne tarehe 30 Juni 2020, wakati anazungumza na wanachama wa chama hicho na viongozi wa CCM waliojitokeza kushuhudia akirejesha fomu za kutetea nafasi ya urais makao makuu ya chama hicho Dodoma.

Hadi leo Jumanne saa 10 jioni, mgombea aliyejitokeza kuchukua fomu upande wa urais wa Tanzania ni yeye pekee huku Zanzibar wakiwa 32.

Hata hivyo, mgombea mmoja, Hussein Ibrahim Makungu amekwisha tangaza kujitoa.

Kati ya hao 31, kuna watoto wa marais wastaafu, viongozi walioko madarakani na wastaafu wanaowania nafasi ya kuingia Ikulu.

Rais Magufuli amesema amekuwa anafuatilia kinachoendelea Zanzibar na kubaini kuna baadhi wameanza kuchafuana mitandaoni.

“Nimeona hiyo dalili kwa wagombea huko Zanzibar,  wengine wanatumia mitandao wanamsema mwenzao, wengine kwenye magazeti lakini atakayechaguliwa ni mmoja tu na Mungu wetu wa mbinguni anamfahamu,” amesema Rais Magufuli.

Mwenyekiti huyo wa CCM amesema “sisi tulikuwa 42 (watia nia kugombea urais wa Tanzania mwaka 2015). Kwa hiyo niwaombe sana hasa wagombea wa CCM Urais wa Zanzibar wakawe waangalifu katika kunadi sera zao. Wasiumizane tunawapa nafasi washindani wetu.”

Rais Magufuli amewataka wanachama 32 waliojitosa katika kinyang’anyiro hicho cha kumrithi Rais Ali Mohamed Shein, anayemaliza muda wake, kuacha kugombana, kwa kuwa kitendo hicho kitaleta mpasuko na kuvipa nguvu vyama vya siasa vya upinzani.

Maudline Cyrus Castico, Waziri wa Kazi, Uwezeshaji Wanawake, Wazee na Watoto Zanzibar akipokea fomu ya kuwania Urais kwa tiketi ya CCM

Amesema, kuna nafasi nyingi za kufanya si lazima urais na chama kitakaposhinda kunakuwa na nafasi Zanzibar na Tanzania hivyo umoja kwa wagombea urais, ubunge, uwakilishi au udiwani ndiyo mafanikio ya chama.

“Katika kipindi hiki cha kampeni, tusikitumie kama kipindi cha kuharibu CCM, sababu tutaenda kule tutaanza kubomoana. Wakati utakapofika wa uchaguzi kugombana na vyama vingine tutakuwa tumeshajiumiza. tukawe wavumilivu,” amesema Rais Magufuli

Wakati huo huo, Rais Magufuli ametoa rai kwa wanachama wa CCM watakaojitokeza kuchukua fomu za kugombea ubunge, uwakilishi na udiwani, kutanguliza maslahi ya chama hicho, badala ya kuweka tamaa ya madaraka mbele.

Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa akipokea fomu ya kuwania Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)

Rais Magufuli amewataka watia nia hao, kuvumiliana katika mchuano huo, huku akiwahimiza kuwaunga mkono wanachama wa CCM watakaofanikiwa kuteuliwa kugombea katika nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi huo.

“Niwaombe kwenye majimbo maana nimeambiwa kuna majimbo yana watia nia 25, mtarogana bure, mtaumiza bure, atakayechaguliwa Mungu anamjua, niwaombe wanachama wa CCM kamwe tusivunje umoja wetu,” amesema

“Tukigombana sana wakati wa kampeni zitatupotezea mwelekeo, tuvumiliane, baada ya uchaguzi atakayechaguliwa tumbebe kwa nguvu zote,” amesema Rais Magufuli.

Waliojitokeza kuwania urais Zanzibar ni;

  1. Mbwana Bakari Juma
  2. Balozi  Ali Abeid Karume
  3. Mbwana Yahya Mwinyi :
  4. Omar Sheha Mussa
  5. Dk. Hussein Ali Mwinyi
  6. Shamsi Vuai Nahodha
  7. Mohammed Jaffar Jumanne
  8. Mohammed Hijja Mohammed
  9. Issa Suleiman Nassor
  10. Profesa Makame Mabarawa
  11. Mwatum Mussa Sultan
  12. Haji Rashid Pandu
  13. Abdulhalim Mohammed Ali
  14. Jecha Salum Jecha
  15. Dk. Khalid Salum Mohammed
  16. Rashid Ali Juma
  17. Khamis Mussa Omar
  18. Mmanga Mjengo Mjawiri
  19. Hamad Yussuf Masauni
  20. Mohammed Aboud Mohammed
  21. Bakari Rashid Bakari
  22. Ayoub Mohammed Mahmoud
  23. Hashim Salum Hashim
  24. Hasna Atai Masound
  25. Fatma Kombo Masound
  26. Iddi Hamadi Iddi
  27. Pereira Ame Silima
  28. Shaame Simai Mcha
  29. Mussa Aboud Jumbe
  30. Mgeni Hassan Juma
  31. Maudline Cyrus Castico

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!