MBWANA Bakari Juma amefungua pazia la uchukuaji wa fomu za kuomba kupitishwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania Urais wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea)
Shughuli ya uchukuaji na urejeshaji wa fomu hizo umeanza leo Jumatatu tarehe 15 hadi 30 Juni, 2020 kwa wanaotaka kugombea urais wa Zanzibar na wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kujitokeza.
Juma amekuwa wa kwanza kufika Ofisi Kuu CCM zilizopo Unguja, Zanzibar. Mara baada ya kukabidhiwa fomu, akasema amejitahimini na kuona anafaa kuwa Rais wa visiwa hivyo.
Amesema, licha ya kuwa Urais ni kazi ngumu lakini hilo litawezekana kwa kudra za Mwenzi Mungu kwani ili atimize majukumu yake lazima we mnyenyekevu, mwadilifu mwenye moyo wa kujitoplea.
Juma amesema, endapo chama hicho kitampitisha na kuwa mgombea urais na Wazanzibar kumpigia kura za kutosha na kuwa Rais, atahakikisha anaweka mbele maslahi ya wananchi.
Amesema, Rais Ali Mohamed Shein, amefanya kazi kubwa nay eye akipitishwa ataendeleza yale aliyoyafanya.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE & MwanaHALISI TV kwa habari zaidi
Leave a comment