Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Urais Z’bar: Mbwana afungua pazia CCM
Habari za Siasa

Urais Z’bar: Mbwana afungua pazia CCM

Mbwana Bakari Juma, kada wa CCM
Spread the love

MBWANA Bakari Juma amefungua pazia la uchukuaji wa fomu za kuomba kupitishwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania Urais wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea)

Shughuli ya uchukuaji na urejeshaji wa fomu hizo umeanza leo Jumatatu tarehe 15 hadi 30 Juni, 2020 kwa wanaotaka kugombea urais wa Zanzibar na wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kujitokeza.

Juma amekuwa wa kwanza kufika Ofisi Kuu CCM zilizopo Unguja, Zanzibar. Mara baada ya kukabidhiwa fomu, akasema amejitahimini na kuona anafaa kuwa Rais wa visiwa hivyo.

Amesema, licha ya kuwa Urais ni kazi ngumu lakini hilo litawezekana kwa kudra za Mwenzi Mungu kwani ili atimize majukumu yake lazima we mnyenyekevu, mwadilifu mwenye moyo wa kujitoplea.

Juma amesema, endapo chama hicho kitampitisha na kuwa mgombea urais na Wazanzibar kumpigia kura za kutosha na kuwa Rais, atahakikisha anaweka mbele maslahi ya wananchi.

Amesema, Rais Ali Mohamed Shein, amefanya kazi kubwa nay eye akipitishwa ataendeleza yale aliyoyafanya.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE & MwanaHALISI TV kwa habari zaidi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!