CHAMA kikuu cha upinzani nchini Zimbabwe ‘Movement for Democratic’ (MDC) kimeenda mahakamani kwa lengo la kukata rufaa, ili kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
MDC imeenda mahakamani ikidai kwamba kulifanyika udanganyifu katika matokeo ya urais yaliyompa ushindi Rais Emmerson Mnangagwa.
Kiongozi wa MDC, Nelson Chamisa amesema timu ya mawakili imefanikiwa kuwasilisha nyaraka za kesi hiyo katika mahakama ya kikatiba.
Chamisa amesema madai yao makuu ni mahakama imtangaze mshindi wa uchaguzi wa rais au iitishe ushaguzi mpya.
Hatua hiyo inakuja baada ya Chamisa kupoteza ushindi kwa kura chache kwenye uchaguzi wa Julai 30 dhidi ya rais wa sasa Emmerson Mnangagwa.
Matokeo ya tume ya uchaguzi yalionyesha kuwa Mnangagwa alipata asilimia 50.8 ya kura akifuatwa na Chamisa akiwa na asilimia 44.3. Lakini Chamisa anadai alipata asilimia 56 ya kura.
Leave a comment