Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Urais wa Mnangagwa wapingwa mahakamani
Kimataifa

Urais wa Mnangagwa wapingwa mahakamani

Spread the love

CHAMA kikuu cha upinzani nchini Zimbabwe ‘Movement for Democratic’ (MDC) kimeenda mahakamani kwa lengo la kukata rufaa, ili kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

MDC imeenda mahakamani ikidai kwamba kulifanyika udanganyifu katika matokeo ya urais yaliyompa ushindi Rais Emmerson Mnangagwa.

Kiongozi wa MDC, Nelson Chamisa amesema timu ya mawakili imefanikiwa kuwasilisha nyaraka za kesi hiyo katika mahakama ya kikatiba.

Chamisa amesema madai yao makuu ni mahakama imtangaze mshindi wa uchaguzi wa rais au iitishe ushaguzi mpya.

Hatua hiyo inakuja baada ya Chamisa kupoteza ushindi kwa kura chache kwenye uchaguzi wa Julai 30 dhidi ya rais wa sasa Emmerson Mnangagwa.

Matokeo ya tume ya uchaguzi yalionyesha kuwa Mnangagwa alipata asilimia 50.8 ya kura akifuatwa na Chamisa akiwa na asilimia 44.3. Lakini Chamisa anadai alipata asilimia 56 ya kura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!