Tuesday , 16 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Urais Chadema: Kesi za Lissu si hoja
Habari za Siasa

Urais Chadema: Kesi za Lissu si hoja

Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu Chadema Bara
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeeleza kwamba hakitakwama kumpitisha Tundu Lissu kwa sababu ya kuhofia kesi zake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Na kwamba, iwapo kura zake zitatosha na Baraza Kuu litaona umuhimu wa kumpitisha Lissu kupeperusha bendera ya chama hicho kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020, basi chama hicho kitasimama naye.

Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu Chadema Bara akizungumza jana tarehe 2 Agosti 2020 na gazeti moja nchini amesema, chama hicho kinatambua kwamba Lissu ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa chama hicho ana kesi kadhaa mahakamani.  

“Tunajua kuwa Lissu ana kesi kadhaa mahakamani, lakini zile ni tuhuma ambazo si kikwazo kwa yeye kugomea urais,” amesema Kigaila.

Amesisitiza kwamba, kesi za Lissu haziwezi kumzuia kupanda kwenye majukwaa na kuomba kura wananchi kwa kuwa, kesi hizo haziitishwi mahamani kila siku.

“Sio kila siku kuna kesi, siku ambazo atahitajika kwenda mahakamani atakwenda, siku ambazo hatohitajika ataendelea na kampeni zake.

“Kwa vyovyote vile inabidi hakimu au jaji aelewe kuna mtu anagombea urais au ubunge ikiwezekana kesi isimame ili akimaliza kampeni ziendelee,” amesema.

Tayari jina la Lissu limepenya katika hatua ya Kamati Kuu iliyoketi jana katika Ukumbi wa Mikutano wa Mliman City. Majina mengine yaliyopenya kati ya matano ya awali ni Lazaro Nyalandu na Dk. Myrose Majinge.

Leo Baraza Kuu la Chadema linaendelea na vikao vyake ili kupitisha jina la mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Visiwani Zanzibar.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Nape: Wanasiasa, wanahabari, wafanyabiashara mteteeni Samia

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,...

Habari za Siasa

CAG: TAWA imegawa vibali vya uwindaji bila idhini ya waziri

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

Habari za Siasa

TAMISEMI yatenga bil. 17.79 kwa ajili uchaguzi serikali za mitaa

Spread the loveWIZARA Ofisi ya Rais-TAMISEMI, imetenga fedha kiasi cha Sh. 17.79...

Habari za Siasa

CAG abaini madudu katika vyama 10 vya upinzani

Spread the loveUKAGUZI wa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!