MAULID Mtulia, Mbunge wa Kinondoni kwa tiketi ya Chama cha Wananchi CUF amejiuzulu uanachama na ubunge kupitia chama hicho kwa madai kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli, anaandika Faki Sosi.
Mtulia amesema amefikia uamuzi huo kwa kuwa mambo yote waliyoahidi tayari yanafanywa vizuri zaidi na CCM hivyo ni vigumu kuwa mpinzani.
Aidha ametanabaisha kuwa kwa sasa ili uwawakilishe wananchi vizuri inabidi uwe CCM kwani ndo kuna sera za kusaidia wananchi kwa sasa. Hivyo imekuwa ikimuwia vigumu kufanya kazi akiwa nje ya CCM.
Mbunge huyo amesema kwa hiari yangu ameamua kujiuzulu uanachama wa CUF na kujiuzulu nafasi zake zote za uongozi nilizokuwa nashikilia kuanzia Desemba 2, 2017.
* Upinzani kupata pigo
Amesema sababu za kuchukua uamuzi huo ni kutokana na uzoefu alioupata kwa miaka miwili ya ubunge ambapo amebaini kuwa Serikali ya CCM inafanya kazi kubwa ya kutekeleza Ilani na imefanya vizuri katika mambo mengi ambayo upinzani waliahidi kuyatekeleza.
Hivyo haoni sababu ya kuendelea kuwa upinzani na badala yake ameona ni vema aungane na juhudi za Serikali kwa kumuunga mkono Rais Magufuli katika kuwaletea wananchi maendeleo na kukabiliana na kero mbalimbali.
Leave a comment