Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Upinzani watangaza ‘vita’ mpya
Habari za Siasa

Upinzani watangaza ‘vita’ mpya

Hashimu Rungwe
Spread the love

VYAMA vinane vya upinzani nchini, vimedhamiria mambo mawili makubwa kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa baadaye mwaka huu na uchaguzi mkuu mwakani. Anaripoti Hamisi Mguta … (endelea).

Vyama hivyo vimedhamiria kufungua keshi ya kudai Tume Huru ya Uchaguzi na pili, kumfunguia mashitaka Adelardus Kilangi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kwa madai ya kupotosha umma.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 22 Mei 2019 na Hashim Rungwe, mwenyekiti wa umoja huo mbele ya wanahabari wakati akiipongeza Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam kuzuia wakurugenzi wa halmashauri za wilaya na jiji nchini kusimamia chaguzi.

“Sio kwamba tunaishia hapo, tunakwenda mbali zaidi. Tunataka Tume Huru ya Uchaguzi kwasababu bila hivyo, itakuwa ni miujiza kwa watu wa upinzani kutangazwa.

“Hatutegemei kama tutatangazwa na hawa watu, tunajipanga kwenda kudai haki ili tupate Tume Huru ya Uchaguzi,” amesema Rungwe huku akitoa wito kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwa na wasimamizi wake uchaguzi.

Miongoni mwa vyama vinavyounda umoja huo ni pamoja na NCCR Mageuzi, NLD, Chadema, CHAUMMA na ACT Wazalendo.

Rungwe amesema, “Kutokana na maamuzi haya yanayoilazimisha NEC kuwa na watendaji wake wa kusimamia uchaguzi, huu ni wakati muafaka kwa wakurugenzi nao kusimamiwa na NEC.”

Rungwe amesema, umoja huo utaendelea kupigania mchakato wa upatikanaji Katiba Mpya itakayoweka mazingira sawa katika uchaguzi.

“Katiba Mpya itaondoa mzizi huu wa fitina, kuna vitu vina udhi, vinatia kichefuchefu lakini utafanyaje?” amesema.

Rungwe amabaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA) amesisitiza dhamira ya kumshitaki Kilangi kwa madai ya upotoshaji kuhusu hukumu ya wakurugenzi kutosimaia uchaguzi iliyotolewa na Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam.

“Sasa tunakabiliwa na propaganda za kupotosha kuhusu haya yaliyoamuliwa na mahakama kuu. Kumekuwepo na jitihada za CCM na serikali kupotosha maamuzi halali ya mahakama.

“Kwanza kuhusu utekelezaji wa hukumu yenyewe, inajaribu kujengwa picha kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ikisema yeye amekata rufaa hivyo hukumu itasimama hadi rufani itakapoamuliwa, “ amesema Rungwe.

Rungwe ambaye Wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania amesema, “ukikata rufaa au ukipata ushindi kwenye ile rufaa kama ulifungwa, unatolewa nje na ukikata rufaa, ukishindwa utarudishwa ndani.

“Sio mtu akikata rufaa hukumu inaisha, AG anajenga picha ya kupotosha wananchi kwamba, hukumu itasimama, hukumu haitasimama.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!