Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Upinzani washinda uchaguzi DRC, Kabila chali
Kimataifa

Upinzani washinda uchaguzi DRC, Kabila chali

Felix Tshisekedi, Rais wa DR Congo
Spread the love

MGOMBEA wa upinzani, Felix Tshisekedi wa Chama cha UDPS ameshinda uchaguzi wa urais nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), tume ya uchaguzi imesema. Vinaripoti vyombo vya kimataifa….(endelea).

Matokeo ya awali yanaonyesha mgombea huyo wa upinzani amemshinda mgombea mwingine wa upinzani Martin Fayulu, pamoja na mgombea aliyekuwa anaungwa mkono na serikali Emmanuel Shadary.

Mkuu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Ceni) Corneille Nangaa, alisema mapema Alhamisi kwamba Tshisekedi alipata asilimia 38.57 ya kura zilizopigwa na “anatangazwa mshindi wa urais mteule.”

Tshisekedi alipata zaidi ya kura milioni saba 7 huku Fayulu akapata kura takriban 6.4 milioni na mgombea anayeungwa mkono na serikali, Emmanuel Ramazani Shadary akipata takriban kura 4.4 milioni.

Tayari tume ya uchaguzi imemtangaza mpinzani kushinda uchaguzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!