Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Upigaji kura TLS wakamilika
Habari MchanganyikoTangulizi

Upigaji kura TLS wakamilika

Tundu Lissu akiwa na mke wake, wakipiga kura zao katika uchaguzi wa TLS jijini Arusha
Spread the love

HAKUNA marefu yasiyo na ncha. Hatimaye vuta nikuvute ya uchaguzi wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS), imehitimishwa leo asubuhi kwa mawakili kupiga kura kuchagua viongozi wao, anaandika Charles William.

Ingawa kuna nafasi nyingi zinazowaniwa, lakini mvutano mkubwa zaidi ni katika nafasi ya Urais wa TLS ambapo wagombea ni wanne akiwemo Tundu Lissu, Godwin Mwapongo, Francis Stolla na Victoria Mandari.

Hapo awali wagombea wa urais walikuwa watano, lakini Lawrance Masha aliyekuwa miongoni mwa wagombea hao alitangaza kujitoa katika uchaguzi huo siku ya jana katika ukumbi wa AICC.

“Natangaza kujitoa ktika nafasi niliyokuwa nagombea, na naomba wote mliokuwa mkiniunga mkono, mpige kura zenu kwa Tundu Lissu,” alisema Masha jana usiku.

Jana usiku, wagombea wote walipewa nafasi ya kujinadi na kuulizwa maswali huku zoezi la kupiga kura likifanyika leo asubuhi.

Akizungumza kwa njia ya simu na MwanaHALISI Online, Peter Kibatala mbaye ni wakili na wakala wa mgombea Tundu Lissu amesema tayari zoezi la kupiga kura limemalizika saa tano kamili asubuhi.

“Hapa ninavyozungumza na wewe tayari zoezi la kupiga kura limemalizika, kwahiyo tunaingia ndani kwenda kuhesabu kura,” amesema.

Alipoulizwa kuhusu muda ambao matokeo yatatangazwa amejibu, “Siwezi kujua, tume ya uchaguzi ndiyo inayotangaza matokeo baada ya kumalizika kwa zoezi la kuhesabu kura kumalizika. Vuteni subira kidogo.”

Mawakili 6,000 walitarajiwa kupiga kura leo asubuhi ili kuwachagua viongozi wao katika nafasi za urais, makamu wa Rais, ujumbe wa Baraza la TLS na zinginezo. Viongozi hao watakiongoza chama hicho kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

error: Content is protected !!