Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Upepo wa CCM wamtesa Lowassa
Habari za Siasa

Upepo wa CCM wamtesa Lowassa

Spread the love

EDWARD Lowassa, Wziri Mkuu Mstaafu ameonesha kuteswa na hama hama ya wapinzani kuelekea Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Faki Sosi…(endelea).

Lowassa ambaye ni Mjumbe Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ameeleza kusikitishwa na kuhama kwa aliyekuwa Mbunge wa Monduli, Monduli Julias Kalanga (Chadema). Kalaga amehamia CCM usiku wa kuamkia Julai 31, 2018.

Hata hivyo Lowassa amesema, umahiri wa Chadema na moto wake kwenye Uchaguzi Mkuu ujao hauzimwi.

Lowasa kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari ameeleza kuwa, CCM imebadili mbinu na kuamua kurubuni wabunge na madiwani wa upinzani kutokana na ‘moto’ wa upinzani uliowashwa mwaka 2015 kwenye kampeni za uchaguzi mkuu.

“Moto ule tuliouwasha 2015 hauwezi hata mara moja kuzimwa na mbinu hizi. Wataondoka kina Kalanga wengi tu lakini kasi ya moto ule jinsi ilivyo sasa ndani ya mioyo ya Watanzania ni ya moto wa kiangazi,” amesema Lowassa na kuongeza;

“Kalanga hakuwa na sababu za msingi za kujiuzulu nafasi yake hiyo ya heshima ya kuwatumikia wananchi wa Monduli nikiwemo mimi. Uamuzi huo umetuhuzunisha na kutuumiza.

“Lakini nawaomba msife moyo hata dakika moja zaidi, kitendo hicho cha Kalanga kizidi kutupa nguvu, ari, hamasa na mori zaidi wa kuendeleza mapambano ya kuitafuta demokrasia na mabadiliko ya kweli.”

Amesema kuwa, kuhama kwenye siasa sio tukio jipya kwenye dunia hivyo sio sababu ya kurudi nyuma kwenye mapambano, “hakuna jipya katika hili, ni kawaida kwa wana siasa duniani kuhama vyama vyao na kubadilishana vijiti.”

Lowassa alihama kutoka CCM na kujiunga Chadema mwaka 2015 kisha kupewa nafasi ya kukiwakilicha chama hicho kama mgombea urais ambapo aliungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).

Vyama vinavyounda UKAWA ni pamoja na Chama cha Wananchi (CUF), Chama cha NCCR-Mageuzi, NLD na Chadema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!