Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Upelelezi wa Lowassa bado pasua kichwa
Habari za SiasaTangulizi

Upelelezi wa Lowassa bado pasua kichwa

Edward Lowassa alipowasili Makao Makuu wa Jeshi la Polisi
Spread the love

JESHI la Polisi Tanzania bado halijakamilisha upelelezi wa tuhuma zinazomkabiri Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, hivyo wamelazimika kumwachia na kumtaka arudi tena baada ya wiki tatu, anaandika Mwandishi Wetu.

Lowassa aliwasili Makao Makuu ya Polisi saa mbili asubuhi kama alivyoagizwa wiki iliyopita na kuingia moja kwa moja kwenye ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Boaz.

Waziri Mkuu huyo wa zamani aliambatana na mkewe, Regina na mwanasheria wake, Peter Kibatala.

https://youtu.be/YnLYXHocwRo

Muda mchache mara baada ya kuwasili, Lowassa alipewa maelekezo kuwa upelelezi haujakamilika hivyo aliruhusiwa kuondoka na kutakiwa kurudi tena kwa DCI baada ya wiki.

Leo ni mara ya nne kwa Lowassa kuripoti hapo akituhumiwa kutoa kauli za kichochezi wakati wa futari iliyoandaliwa Juni 23, na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara.

Katika futari hiyo, Lowassa anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi kuhusu masheikh wa Taasisi ya Uamsho wanaoshikiliwa gerezani akidai utaratibu wa kisheria ufanyike ili waachiwe huru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!