IDADI ya wagonjwa waliofanyiwa huduma ya kupandikizaa figo katika hospitali ya Taifa Muhimbili imefikia 19 tangu kuanzishwa kwa huduma hiyo mwaka 2017. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).
Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Huduma za Tiba katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Hedwiga Swai amesema kuwa utoaji wa huduma hiyo ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya awamu ya tano ya kupunguza rufaa za wagonjwa kwenda nje ya nchi kwa matibabu ambayo yalikuwa hayatilewi ndani ya nchi.
“Tayari wataalam wetu wa ndani hususan madaktari bingwa wamepata ujuzi wa kufanya upandikizaji wa figo kwa kiwango cha asilimia 75 huku asilimia 25 wakielekezwa na wataalam kutoka nje,” amesema.
Aidha Dkt. Swai amesema kuwa wanaahidi kufanya upandikizaji kwa angalau watu watano kwa mwezi ikiwa ni mpango wa muda mfupi kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu ambapo mpango wao wa kila siku ni kufanya upandikizaji kwa mgonjwa mmoja kila siku ambayo ni sawa na wagonjwa 20 kwa mwezi ambapo watakuwa wagonjwa 200 au 240 kwa mwaka.
Leave a comment