Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa UN waumizwa na uamuzi wa TZ
Habari za Siasa

UN waumizwa na uamuzi wa TZ

Balozi Augustine Mahiga, Waziri wa Katiba na Sheria
Spread the love

TUME ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa (UN), imeitoa wito kwa Serikali ya Tanzania kutathimini upya, uamuzi wake wa kuzuia asasi za kiraia na raia, kufungua kesi kwenye Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu (AfCHPR). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tume hiyo imetoa wito huo jana tarehe 3 Desemba 2019 kupitia ukurasa wake wa twitter.

Taarifa ya tume hiyo imeeleza kuwa, mahakama ni muhimu katika mchakato wa haki na uwajibikaji nchini Tanzania.

“Tumeumizwa na uamuzi wa serikali ya Tanzania kuzuia mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s), kupeleka kesi katika Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu.

Tunahimiza serikali kufikiria tena. Mahakama ni muhimu kwa haki na uwajibakaji nchini Tanzania,” inaeleza taarifa ya tume hiyo.

Madai ya Tanzania kutaka kujitoa katika mahakama hiyo yaliibuka hivi karibuni, na kupeleka Balozi Augustine Mahiga, Waziri wa Katiba na Sheria kutoa ufafanuzi wa suala hilo.

Katika ufafanuzi wake, Balozi Mahiga alisema Tanzania haijajitoa, bali imeomba kubadilisha itifaki kwenye mahakama hiyo, kwa madai kwamba inakinzana na sheria za Tanzania.

Balozi Mahiga alisisitiza kwamba, kama itifaki hiyo ambayo hakuihataja, haitarekebishwa, Tanzania itajitoa kwenye mahakama hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!