Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Umeme kukatika Dar es Salaam
Habari Mchanganyiko

Umeme kukatika Dar es Salaam

Mafundi umeme wakiwa kazini
Spread the love

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO), limetangaza katizo la umeme katika baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Ilala na Temeke, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa tangazo hilo, katizo hilo litatokea kesho tarehe 22 Oktoba 2019, kuanzia saa 2:30 asubuhi hadi 10:30 jioni, kwenye njia ya Msongo wa 132KV ili kuruhusu kazi ya kuungwa kebo ya Transfoma mpya.

Tangazo hilo limeeleza kuwa, Transfoma hiyo mpya ina uwezo mkubwa wa Megawati 300MVA, ambayo itasaidia kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme kwa Jiji la Dar es Salaam, Zanzibar na Pwani.

Maeneo yatakayokumbwa na katizo hilo ni pamoja na, Buguruni, Vingunguti, Tazara, Gongo la Mboto, Ukonga, Mombasa, Mzambarauni, Pugu.

Maeneo mengine ni Yombo, Kitunda, Machimbo, Mwanagati, Mbondole pamoja na baadhi ya maeneo ya Tabata.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

error: Content is protected !!