Wah. Viongozi na Wabunge!
Amani iwe kwenu wote!
Ujenzi wa Demokrasia ni safari ndefu yenye milima, mabonde, miiba, mawe na kila aina ya majaribu yenye vikwazo.
Waasisi wa Chama walifananisha na safari ya treni toka Dar kwenda Kigoma. Kwamba kuna watakaoshuka njiani kwa sababu mbalimbali, (halali na batili) hali kadhalika wengine wengi watapanda vituo mbalimbali kuungana na safari.
Hampaswi kushangaa baadhi yetu kuishia njiani. Nina hakika na imani kuwa hatakuwa wa mwisho kutoka.
Yumkini wako maelfu ambao wanapanda treni yetu kila siku.
Si kila atokaye ni hasara kwa Chama. Kutoka kwingine kwaweza kuwa baraka.
Wajibu huu wataka moyo Mkuu!! Shime wenye nia ya kufika Kigoma kwa umoja wetu tusonge mbele tukijiamini sana!!
Freeman Mbowe (MP)
Mwenyekiti & KUB
Leave a comment