Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uhujumu uchumi: Waliotuma maombi kwa DPP watajwa
Habari za SiasaTangulizi

Uhujumu uchumi: Waliotuma maombi kwa DPP watajwa

Dk. Ringo Tenga, Mkurugenzi na Mwanasheria wa Kampuni ya Mawasiliano ya Six Telecoms Limited (katikati) akiwa mahakamani Kisutu
Spread the love

MAJINA ya watuhumiwa wa kesi ya uhujumu uchumi nchini, waliomwandikia Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), Biswalo Mganga yameanza kutajwa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Tayari Dk Ringo Tenga, Mkurugenzi na Mwanasheria wa Kampuni ya Mawasiliano ya Six Telecoms Limited, ni miongoni mwa watuhumiwa ambao tayari wameandika barua ya kukiri na kuomba afueni.

Byrson Shayo ambaye ni wakili wa Dk. Tenga  leo tarehe 27 Septemba 2019, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakati ilipotajwa kesi hiyo.

Dk. Ringo akiwa na wenzake, wanakabiliwa na mashtaka sita ikiwa ni pamoja na tuhumza za utakatishaji fedha jambo lililoisababisha hasara Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) hasara zaidi ya Dola za Marekani 3,748,751.

Watuhumiwa wengine ambao wamemwandiki barua DPP ni pamoja na Mfanyabiashara na Mkurugenzi wa kampuni hiyo Peter Noni, Mkuu wa fedha wa kampuni hiyo Noel Chacha na Rashidi Shamte ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo.

Kwa mara ya kwanza Dk. Tenga na wenzake walifikisha mahakamani tarehe 20 Novemba 2017 wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!