Tuesday , 16 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ugonjwa wa ajabu watesa wanafunzi Tanga
Habari MchanganyikoTangulizi

Ugonjwa wa ajabu watesa wanafunzi Tanga

Spread the love

WANAFUNZI wanaosoma shule ya sekondari ya Kwamkabara kata ya Kwamkabara wilayani Muheza mkoani Tanga wamepatwa na ugonjwa wa ajabu unaosababisha kuanguka hovyo, anaandika Mwandishi Wetu.

Ugonjwa huo umesababisha wanafunzi 52 mpaka 70  wanaanguka baada ya kushikwa na ugonjwa waajabu wa kuanguka na kupiga kelele pamoja na kutokwa ute mdomoni kama wamepandisha mashetani.

Tukio hilo limetokea juzi katika shule hiyo ya sekondari ya kata ya Kwamkabara wilayani Muheza mkoani Tanga. Mkuu wa shule hiyo Getrude Moyo amethibitisha kuwapo tukio hilo la watoto kuanguka na kupiga kelele.

Akizungumza eneo la tukio Ofisa elimu wa shule za msingi wilayani Muheza, Julitha Akko amesema kuwa wanafunzi hao walishikwa na ugonjwa wa kuanguka na kupiga kelele kama wamepandisha mashetani.

Akko alisema kuwa mpaka sasa chanzo cha wanafunzi hao kuanguka na kupiga kelele bado hakijafahamika na wazazi kwa kushirikiana na walimu wa shule hiyo walifanya maombi ya kukemea mapepo  katika shule hiyo na baadae wanafunzi hao kuchukuliwa na kurudi nyumbani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

Habari Mchanganyiko

Sekta binafsi yasifu utekelezaji wa Mkumbi

Spread the loveSERIKAL imepongezwa kwa utekelezaji wa mapendekezo ya sekta binafsi kupitia...

Habari Mchanganyiko

Kamati ya bunge yapigia chapuo kilimo ikolojia

Spread the loveSERIKALI kupitia Wizara ya Kilimo imeshauriwa kushirikiana na wadau wa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yapata hasara 113 milioni hospitali kuwapa misamaha wagonjwa wasiostahili

Spread the loveSERIKALI imepata hasara ya kiasi cha Sh. 111.76 milioni, baada...

error: Content is protected !!