Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Uganda yapiga marufuku kampeni za majukwaani
Kimataifa

Uganda yapiga marufuku kampeni za majukwaani

Bobi Wine
Spread the love

TUME ya Uchaguzi ya Uganda imepiga marufuku mikusanyiko ya kampeni za jukwaani na kuagiza, kampeni za uchaguzi mkuu zifanyike kupitia vyombo vya habari. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Kwenye uchaguzi huo miezi sita ijayo, Uganda inatarajia kuchagua rais, wabunge na wawakilishi wa ngazi za chini. Uchaguzihuo unatarajiwa kufanyika Januari 2021.

Tume hiyo imeeleza, imechukua hatua hiyo kuhakikisha virusi vya corona havipati nafasi ya kusambaa kutokana na mikusanyiko hiyo, hivyo kuliingiza taifa kwenye janga.

Taarifa ya tume hiyo imeeleza, utaratibu wa sasa wa uvaaji barakoa, umbali unakubalika na njia zingine zinazotumika kujiepusha na maambukizi hayo, zitasimamiwa siku ya upigaji kura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!