Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uchaguzi Z’bar wamponza mtoto wa Chacha Wangwe
Habari za SiasaTangulizi

Uchaguzi Z’bar wamponza mtoto wa Chacha Wangwe

Bob Chacha Wangwe (katikati) akiwasili mahakamani Kisutu
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhuku kwenda jela mwaka mmoja  na nusu au kulipa faini ya Sh. 5 milioni, mtoto wa Marehemu Chacha Wangwe, Bob baada ya kukutwa na hatia kutumia vibaya mtandao, anaandika Faki Sosi.

Hukumu hiyo imetolewa leo Novemba 15, 2017 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Huruma Shahidi ambapo alisema kuwa mtuhumiwa huyo anahatia ya kutumia vibaya mtandao wa kijamii kutokana na upotoshaji alioufanya.

Bob Wangwe alitoa maoni yake kwenye ukurasa wake wa Facebook kuhusu uchaguzi wa marudio wa Zanzibar uliofanyika Machi 20, 2016.

Kwenye kesi hiyo namba 167 ya mwaka 2016, Bob Chacha Wangwe alidaiwa kutenda kosa hilo Machi 15, 2016 kwa kuchapicha maneno haya: “Tanzania ni ambayo….inajaza chuki wananchi … matokeo ya kubaka demokrasia Zanzibar ni hatari zaidi ya Muungano wenyewe…. Haiwezekani nchi ya Zanzibar kuwa koloni la Tanzania Bara kwa sababu za kijinga.”

Wakati wa usikilizwaji wa kesi hiyo upande wa Jamhuri ulileta mahakamani hapo mashahidi sita huku upande wa utetezi shahidi alikuwa mmoja ambaye ni mshitakiwa mwenyewe.

Awali Bob alipandishwa kizimbani Mei 11, 2016 kwa tuhuma za kuchapisha taarifa za upotoshaji kwenye ukurasa wake wa wa Facebook.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

error: Content is protected !!