Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uchaguzi  wavuruga UVCCM Mwanza 
Habari za Siasa

Uchaguzi  wavuruga UVCCM Mwanza 

Umoja wa Vijana CCM (UVCCM)
Spread the love

UCHAGUZI wa marudio wa kumtafuta mwenyekiti mpya wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM (UVCCM), katika wilaya ya Nyamagana jijini Dar es Salaam zimegubikwa vurugu, anaandika Hamis Mguta.

Vurugu hizo vimeibuka baada ya wajumbe kutoka Kata ya Mahina kuzuiwa kuingia ukumbini kupiga kura kwa madai ya kuwa si wajumbe halali.

Katibu wa wajumbe hao, Samora Msiba amesema baada ya kuhoji sababu ya wao kuzuiwa kuingia ukumbini walielezwa kiongozi wao wa kata hana mawasiliano au mahusiano mazuri na serikali.

“Tunaomba viongozi wa ngazi za juu waliangalie suala hili kwa kuwa hata sisi tuna haki ya kupiga kura na si kusukumwa na kususiwa ovyo kwa kuhusishwa na kesi zisizotuhusu,” amesema Msiba.

Hata hivyo, chanzo chetu kinaeleza kuwa vurugu zimesababisha walinzi wa chama hicho (Green Guard) kuzuiwa kufanya kazi yao na badala yake mgambo wa Jiji la Mwanza kusimamia uchaguzi huo.

Kuhusu kuzuiliwa kwa walinzi hao wa Green Guard, Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Mahina ambaye pia ni Katibu wa Green Guard wilayani humo Kagambo Paul amesema amekerwa na kitendo cha kuporwa jukumu lake la kusimamia uchaguzi na kupewa jeshi la akiba la mgambo.

Uchaguzi kwa mara ya kwanza ulifanyika Septemba 23 ambao mshindi hakupatikana kutokana na kura kutofikia nusu ya zilizopigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!