Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Uchaguzi TLS, Dk. Mwakyembe aanza kupukutika
Habari MchanganyikoTangulizi

Uchaguzi TLS, Dk. Mwakyembe aanza kupukutika

Harrison Mwanyembe, Waziri wa Katiba na Sheria Tanzania
Spread the love

WAZIRI wa Sheria na Katiba, Dk. Harrison Mwakyembe, siyo mjumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) na hivyo hataweza kupiga kura, anaandika Saed Kubenea.

Dk. Mwakyembe ambaye ni wakili wa mahakama kuu, hataruhusiwa kupiga kura kwa kuwa hayumo kwenye orodha ya mawakili walioidhinishwa na Jaji mkuu kwa mwaka huu.

Taarifa zinasema, Dk. Mwakyembe hakuidhinishwa kuwa wakili kutokana na kushindwa kulipa ada zake za kila mwaka kama ilivyoekezwa na sheria za nchi na kanuni za TLS.

Katika siku za hivi karibuni, Dk. Mwakyembe amekuwa akitoa kauli tata kupinga chama hicho kupitisha wagombea anaodai ni wanasiasa na kusema, “hilo likitokea, serikali haitasita kuifuta TLS.”

Dk. Mwakyembe hajamtaja mwana taaluma ambaye ni mwanasiasa na ambaye anataka kugombea urais wa chama hicho.

Hata hivyo, anayeonekana kulengwa na Dk . Mwakyembe, ni Tundu Lissu, wakili machachari nchini, mbunge wa Singida Mashariki na mwanasheria mkuu wa Chama cha Demokrsia na Maendeleo ( Chadema).

Lissu, ni miongoni mwa wagombea wanne wa wanafasi ya Rais wa TLS.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

error: Content is protected !!