Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uchaguzi Mkuu 2020: Takukuru yamtia mbaroni Aden Rage
Habari za SiasaTangulizi

Uchaguzi Mkuu 2020: Takukuru yamtia mbaroni Aden Rage

Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Tabora nchini Tanzania, inamshikilia Ismail Aden Rage kwa tuhuma za rushwa na kuanza kampeni kabla ya wakati za uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora … (endelea).

Rage alishikiliwa na Takukuru kuanzia tarehe 23 hadi 24 Mei, 2020 alipoachiwa kwa dhamana baada ya taasisi hiyo, kupokea taarifa kuwa Mkurugenzi huyo wa Voice of Tabora FM aliwakusanya viongozi wa kata na matawi wa CCM kwa lengo la kuwashawishi wampigie kura.

Taarifa ya Mussa Chaulo, Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Tabora aliyoitoa leo Jumatatu tarehe 25 Mei, 2020 imesema uchunguzi wa suala hilo unaendelea.

Chaulo amewaonya wale wote walioanza kujipitisha ili kufanya ushawishi kwa wanachama ili wawachagua watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Rage aliwahi kuwa mbunge wa Tabora Mjini kupitia CCM kati ya mwaka 2010 na 2015.

Pia, amewahi kuwa Rais wa klabu ya Simba ya Jijini Dar es Salaam

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!