TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) nchini Tanzania, imebainisha mambo matatu yasiyopaswa kufanywa na Serikali wakati wa Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).
NEC imebainisha mambo hayo kupitia kitabu chake cha Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2020.
Mambo hayo ni; vyombo vya ulinzi na usalama kutumia madaraka yao kukandamiza wagombea, wafuasi au chama chochote cha siasa.
Aidha, vyombo hivyo vitekeleze majukumu yake kwa weledi.
Soma zaidi:-
Pili; kuingilia au kuzuia isivyo halali mikutano iliyoitishwa na vyama vya siasa au wagombea kwa mujibu wa ratiba za uchaguzi.
Tatu; kumhamisha mtumishi yeyote wa Serikali anayehusika na shughuli za uchaguzi mpaka mchakato wa uchaguzi ukamilike.
Endapo Serikali itaona kuna ulazima wa kumhamisha mtumishi kama huyo ni lazima ishauriane na NEC.
Endelea kufuatilia MwanaHalisi Online, MwanaHalisi TV na mitandao yetu ya kijamii Facebook, Twitter na Instagram kwa habari na taarifa mbalimbali.
Leave a comment