Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Ubingwa ‘La Liga’ Madrid yatawazwa rasmi
Michezo

Ubingwa ‘La Liga’ Madrid yatawazwa rasmi

Spread the love

KLABU ya Real Madrid ya Hispania jana ilitangwazwa mabingwa wapya wa Ligi kuu nchini humo (La Liga), baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Villarreal na kufikisha alama 86, ambazao haziwezi kufikiwa na timu yoyote kwenye Ligi hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… endelea

Madrid inachukua taji hilo kwa mara 34 katika historia huku ikifuatiwa na Fc Barcelona nafasi ya pili yenye pointi 79 baada ya kupoteza kwenye mchezo wa jana dhidi ya Osasuna kwa mabao 2-1, huku kila timu ikibakiwa na michezo miwili.

Baada ya kutwaa ubingwa huo Madrid inabakiwa kuwa klabu inayoongoza kwa kutwaa kombe hilo mara nyingi nchini Hispania chini ya kocha wake Zinedine Zidane ambaye ametwaa taji hilo mara mbili.

Taji hilo linakuwa la 11 kwa kocha huyo toka alipoaanza kukinoa kikosi hicho Januari, 2016 na baadae kurejea tena Machi, 2019 na kuwa mmoja wa kocha mwenye mafanikio zaidi kwa kutwaa jumla ya mataji 11, klabuni hapo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!