Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tundu Lissu aibwaga serikali, apata dhamana
Habari za SiasaTangulizi

Tundu Lissu aibwaga serikali, apata dhamana

Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema na Mbunge wa Singida (katikati), akiinga ndani ya chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu
Spread the love

TUNDU Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, hatimaye amepata dhamana baada ya ombi la mawakili wa serikali la kuomba mahakam imnyime dhamana kutupiliwa mbali, anaandika Hellen Sisya.

Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri amesema, baada ya kupitia hoja za serikali na majibu ya mawakili wa utetezi, haoni mantiki ya kuzuia dhamana kwa Lissu.

Hivyo, Hakimu Mashauri amemtaka Lissu kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambapo kila mmoja atasaini bondi ya Sh. 10 milioni.

Lissu ametimiza masharti hayo na kuachiwa kwa dhamana, lakini anatakiwa kupewa kibali cha mahakama kila anapotaka kutoka nje ya Dar es Salaam.

Kesi itasikilizwa Agosti 24, 2017 na upande wa serikali imesema upepelezi wa kesi hiyo umekamilika.
Baada ya kuachiwa Lissu na mawakili wake wamezuiwa kuzungumza nje ya mahakama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!