MTANDAO wa MwanaHALISI unaopatikana kupitia www.mwanahalisionline.com umererejea tena mtaani kwa wasomaji wake. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Hii ni baada ya kukamilisha taratibu zote zinazohitajika za kupata leseni ya kurusha taarifa zake mitandaoni.
Kufuatia hatua hiyo kubwa, uongozi wa kampuni ya Hali Halisi Pubilishers Limited (HHPL), unaomiliki mtandao huo pamoja na ule wa MwanaHALISI Forum, unaahidi kuendelea kuwaletea wasomaji wake taarifa sahihi na za kweli.
Aidha, kufuatia kuvuka katika tundu hilo, tunatarajia kujiimarisha zaidi kwa kuongeza uzalishaji, ikiwamo kuripoti matukio mbalimbali kwa haraka na kwa usahihi.
Tunawatakia usomaji mwema.
Robert Katula,
Meneja Mkuu,
HHPL
Leave a comment