Wednesday , 17 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Tume ya Uchaguzi Kenya yazidi kusambaratika.
Kimataifa

Tume ya Uchaguzi Kenya yazidi kusambaratika.

Ezra Chiloba, Mtendaji Mkuu wa Tume ya Uchaguzi ya Kenya (IEBC)
Spread the love

OFISA Mkuu Mtendaji wa Tume ya Uchaguzi Nchini Kenya, Ezra Chiloba anatarajiwa kuchukuwa likizo ya wiki tatu na hatoshiriki katika uchaguzi wa marudio utakaofanyika wiki ijayo Oktoba 26 mwaka huu.

Taarifa kutoka ndani ya IEBC zinasema, Chiloba amefanya uamuzi huo wa kibinafsi wa kutoshiriki ili kujenga upya imani ya washikadau ambao wamelalamika kuhusu maofisa wa tume hiyo.

Ofisa huyo amekuwa chini ya shinikizo kubwa kutoka muungano wa upinzani Nasa kujiuzulu, huku mgombea wa urais wa muungano huo Raila Odinga akiitisha maandamano ya kumlazimisha kuondoka pamoja na maofisa wengine ikiwatuhumu kusimamia vibaya uchaguzi wa Agosti 8 ambapo rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi.

Matokeo ya uchaguzi huo hata hivyo yalifutwa na mahakama ya juu kwa kuzingatia sheria.
Chiloba anachukua likizo baada ya mwenyekiti wa tume hiyo, Wafula Chebukati kutaka maofisa waliotajwa baada ya uchaguzi huo wasiache kazi.

Mahakama ya juu ilisema kuwa haikupata ushahidi kuhusu makosa yaliofanywa na maofisa hao, lakini wanasiasa wamelalamika na kuishutumu tume hiyo kwa kujaribu kufanya udanganyifu katika uchaguzi huo mbali na wizi wa kura.

Uamuzi huo wa kuchukua likizo ulijadiliwa na mwenyekiti na anaamini kwamba kutokuwepo kwake hakutaathiri maandalizi ya tume hiyo kusimamia uchaguzi ulio huru na haki .

Ofisa mwingine, Dk. Roselyn Akombe amejiuzuru kazi katika tume hiyo kwa madai kwamba chombo hicho hakiwezi kufanya uchaguzi ulio huru na haki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

Habari za SiasaKimataifa

Rais Faye amteua aliyekuwa mfungwa mwenzie kuwa waziri mkuu

Spread the loveRais mpya wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, amemteua Ousmane Sonko...

error: Content is protected !!