ZIARA ya Rais John Magufuli katika gereza kuu la Butimba jijini Mwanza, imeibua tuhuma nzito. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Kalikenya Nyamboge, mfungwa anayetumikia kifungo cha miaka 30 kwenye gereza hilo, mbele ya Rais Magufuli ameibua kwamba, gerezaji hapo ukichomwa sindano, unakufa huku wengine kuporwa mali na maofisa wa gereza hilo.
Hata hivyo, amemweleza rais kuwa, kwa sasa vifo vya wafungwa vimepungua baada ya Jenerali Kamishna (hakumtaja jina) kupeleka mganga msomi mpya.
“Na si mara ya kwanza wao kuua mimi nilikuwa nimepanga nikitoka nije kukwambia na nikitoka nitakuletea mambo yote yanayotokea huku, lakini huyu usimuache maana kwa Mwenyezi Mungu utakua umeandika maelezo ya mauji,” amenukuliwa Nyamboge.
Mfungwa huyo anamthibitishia Rais Magufuli kwamba, kwenye gereza hilo, vitendo vya ajabu vimekuwa vikifanywa na maofisa wa magereza.
Akizungumza madhila gereza hilo, Nyamboge amemtaja ofisa wa usalama wa gereza hilo kuwa kikwazo na mnyanyasaji akidai kuwa, huwapa wafungwa simu kisha wakikutwa nazo baada ya msako huporwa kila kitu.
Akizungumzia wasiwasi wa usalama wake Nyamboge amemwomba Rais Magufuli kuondoka na ofisa huyo kwa kuwa, anaweza kumdhuru endapo atamwacha.
“Mheshimiwa rais, huyu ofisa akupe mihuri na hizo simu uondoke nazo, utajua mwenyewe utaenda kufanyia nini na ikibidi ondoka naye kwani ukifanya hivyo utakiwa umetusaidia sana na ukimuacha atanidhuru,” amesema Nyamboge.
Rais Magufuli yupo ziarani Mwanza ambapo leo tarehe 16 Julai 2019, ametembelea gerezani kuu la Butimba.
Leave a comment