Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tuhuma nzito ziara ya Rais Magufuli
Habari za Siasa

Tuhuma nzito ziara ya Rais Magufuli

Spread the love

ZIARA ya Rais John Magufuli katika gereza kuu la Butimba jijini Mwanza, imeibua tuhuma nzito. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kalikenya Nyamboge, mfungwa anayetumikia kifungo cha miaka 30 kwenye gereza hilo, mbele ya Rais Magufuli ameibua kwamba, gerezaji hapo ukichomwa sindano, unakufa huku wengine kuporwa mali na maofisa wa gereza hilo.

Hata hivyo, amemweleza rais kuwa, kwa sasa vifo vya wafungwa vimepungua baada ya Jenerali Kamishna (hakumtaja jina) kupeleka mganga msomi mpya.

“Na si mara ya kwanza wao kuua mimi nilikuwa nimepanga nikitoka nije kukwambia na nikitoka nitakuletea mambo yote yanayotokea huku, lakini huyu usimuache maana kwa Mwenyezi Mungu utakua umeandika maelezo ya mauji,” amenukuliwa Nyamboge.

Mfungwa huyo anamthibitishia Rais Magufuli kwamba, kwenye gereza hilo, vitendo vya ajabu vimekuwa vikifanywa na maofisa wa magereza.

Akizungumza madhila gereza hilo, Nyamboge amemtaja ofisa wa usalama wa gereza hilo kuwa kikwazo na mnyanyasaji akidai kuwa, huwapa wafungwa simu kisha wakikutwa nazo baada ya msako huporwa kila kitu.

Akizungumzia wasiwasi wa usalama wake Nyamboge amemwomba Rais Magufuli kuondoka na ofisa huyo kwa kuwa, anaweza kumdhuru endapo atamwacha.

“Mheshimiwa rais, huyu ofisa akupe mihuri na hizo simu uondoke nazo, utajua mwenyewe utaenda kufanyia nini na ikibidi ondoka naye kwani ukifanya hivyo utakiwa umetusaidia sana na ukimuacha atanidhuru,” amesema Nyamboge.

Rais Magufuli yupo ziarani Mwanza ambapo leo tarehe 16 Julai 2019, ametembelea gerezani kuu la Butimba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!