DONALD Trump, Rais wa Marekani ‘amezingirwa’ na sasa amesema, “nitakabidhi madaraka kwa amani.’ Inaripoti mitandaoya kimataifa…(endelea).
Kwa mara ya kwanza tangu kufanyika Uchaguzi Mkuu nchini humo, Trump amekiri kushindwa kwenye uchaguzi huo na sasa anajiandaa kuondoka.
Kiongozi huyo ‘mtata’ kwenye video yake aliyoiweka jana jioni Alhamisi ya tarehe 7 Januari 2021, amesema “niko tayari kukabidhi kwa amani.”
Katika video hiyo, hakutaja kabisa kuhusu madai yake ya awali ya kuibiwa kura ambayo yaliwachochea wafuasi wake kupiga kambi nje ya Ikulu ya Whitehouse na kuvamia Jengo la Capitol.
Wakati akitoa matamshi hayo, viongozi wa Chama cha Demokratik cha rais mteule wa taifa hilo, Joe Biden kinashinikiza Trump kung’olewa kwenye ofisi hiyo kabla ya muda kufika.
Soma zaidi hapa
Bunge la Marekani lavamiwa, risasi zarindima
Hoja zinazoporomshwa na vingozi hao ni kwamba, amekuwa akichochea wananchi kufanya uasi na vurugu hivyo kuligharimu Taifa hilo.
Baada ya saa 12 za kifungo cha ukurasa wake wa twitter, tayari mtandao huo umemfungulia ambapo ametumia ukurasa huo kulaumu wafuasi wake kwa uvamizi wa jengo hilo.
“Ni shambulio baya la waandamanaji waliovamia Bunge la Congress,” ameandika Trump.
Katika kanda hiyo mpya ya video alisema “sasa Bunge la Congress limeidhinisha matokeo na sasa utawala mpya utaingia tarehe 20 Januari.”
“Lengo langu sasa ni kuhakikisha kuwa mchakato wa kukabidhi madaraka unafanyika kwa njia ya amani. ‘Wakati huu tunahitaji maridhiano.”
Leave a comment