Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Trump amejifunza kwa Bush?
Kimataifa

Trump amejifunza kwa Bush?

Donald Trump, Rais wa Marekani
Spread the love

KAMA mji au jimbo litashindwa kuchukua hatua muhimu za kurejesha hali ya amani, basi nitatumia jeshi la Marekani kufanya kazi hiyo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Ni kauli ya Donald Trump, Rais wa Marekani inayojadiliwa kwa sasa hususan baada ya magavana kueleza, Rais huyo hana mamlaka hayo kisheria.

Ametoa kauli hiyo baada ya maandamano, vurugu na uporaji kushika kasi nchini humo, kutokana na polisi wa Minnesota kufanya mauaji ya Mmarekani mweusi George Floyd wiki iliyopita.

Swali linabaki, je Trump anaweza kuchukua hatua hiyo na iliwahi kuchukuliwa na rais yeyote kabla yake?

Robert Chesney, Profesa wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Texas anasema, Trump anaweza kufanya hivyo na kwamba hatokuwa Rais wa kwanza kutumia jeshi ndani ya mipaka ya nchi hiyo.

Anafafanua, mwaka 1807 Marekani ilipitisha sheria kuruhusu Rais wa taifa hilo kutumia jeshi bila mamlaka za majimbo, na kwamba ila sharti ya kuwepo kwa hali ya hatari.

Akieleza chanzo cha kuundwa kwa sheria hiyo, Profesa Chesney amesema, mwaka huo yalitokea mashambulizi ya raia wa India.

“Sheria hiyo inasema, ridhaa ya magavana haitakiwi pale Rais anapothibitisha kuwa hali katika jimbo inawia ngumu kusimamia sheria nchini Marekani, au wakati haki za raia zinapotishiwa,” amesema.

Pia amesema, ipo sheria iliyopitishwa mwaka 1878 ikitaka mamlaka ya Bunge kuidhinisha matumizi ya jeshii, “lakini kuna sheria ya kupambana na vitendo vya uvamizi ina nguvu ya kusimama yenyewe, Rais huwa na mamlaka kisheria kupeleka jeshi bila kuomba idhini kutoka kwenye majimbo katika mazingira ya sasa.”

Kwa mujibu wa huduma ya utafiti ya bunge, sheria hii iliwahi kutumika mara kadhaa zamani, ingawa si kwa takribani miongo mitatu.

Tangu kupitishwa kwake, mara ya kwanza ilitumiwa na Rais mstaafu George HW Bush mwaka 1992 wakati wa vurugu za mji kwenye Los Angeles.

Mwaka 1957 Rais Dwight Eisenhower alitumia sheria hiyo lakini alikumbana na upinzani mkubwa kutoka kwa magavana.

Yeye alipeleka jeshi Arkansas kudhibiti maandamano ya wanafunzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!