Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Trump agonga mwamba, wahamiaji wapeta 
Kimataifa

Trump agonga mwamba, wahamiaji wapeta 

Spread the love

ZUIO la wahamiaji kuingia nchini Marekani lililotolewa na Donald Trump, rais wa nchi hiyo limefutwa, anaandika Wolfram Mwalongo.

Hatua hiyo imetajwa kuwa kigingi cha kwanza katika utawala wa Trump ambapo rais huyo amevuruga uhusiano wa kidiplomasia na mataifa ya nje.

Ni kutokana na uamuzi wa kutopokea wahamiaji hususani wanaotoka mataifa ya Kiislamu.

Kwa sasa wahamiaji wataendelea kuingia kwenye taifa hilo kutokana na zuio la mahakama mpaka pale kesi hiyo itakapofika tamati.

Aidha, hatua ya kiongozi huyo kufuta visa (vibali vya kuishi) katika taifa hilo kwa raia kutoka mataifa ya Kiislam, imetajwa kama ukikwaji wa haki na kinyume na sheria za nchi hiyo.

Taarifa kutoka ndani ya Ofisi ya Bob Ferguson’s , Mwanasheria Mkuu nchini Marekani zimesema kwamba, hakuna aliye juu ya sheria hivyo hata akiwa rais anapaswa kufuata sheria.

“Katiba imeshinda leo hii, hakuna aliye juu ya sheria hata akiwa rais,”amesema Ferguson’s.

Rais Trump amesaini sheria hiyo Januari 27 ambapo alisema, lengo ni kuondoa raia wanaotoka mataifa ya Kiislamu ndani ya miezi mitatu.

Alidai kitendo hicho kitaliwezesha taifa lake kubaki salama dhidi ya ugaidi ambapo ncchi hizo ni Iraq, Syria, Sudan, Iran, Somalia, Libya na Yemen.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!