Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tisa mbaroni kwa mauaji ya watoto wa familia moja
Habari Mchanganyiko

Tisa mbaroni kwa mauaji ya watoto wa familia moja

Pingu
Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Kagera linawashikilia watu tisa wanaoshukiwa kuhusika na tukio la kuwauwa kinyama watoto wawili wa familia moja na kuwatupa kichakani kwenye kijiji cha Mashule wilaya ya Bukoba. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari mapema leo tarehe 23 Oktoba 2018, Kaimu Kamanda wa Polisi Kagera, Issack Msengi ameeleza kuwa, mauaji ya watoto hao, Auson Respikius (7) na Alistidia Respikius (5) yanahusishwa na imani za kishirikina.

“Mauaji haya ya watoto yanahusishwa na imani za kishirikina na mpaka sasa tunawashikilia watu Tisa kuhusiana na tukio hilo,” amesema Kamanda Msengi.

Kwa mujibu wa Baba wa watoto hao, John Respikius anadai kuwa watoto wake walipotea tangu Jumapili tarehe 21 Oktoba 2018 ambapo jana miili yao ilipatikana kichakani ikiwa imechinjwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!