IKIWA zimebaki siku tatu kabla ya michuano ya vijana ya kufuzu fainali za Afrika chini ya umri wa miaka 17, katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kuanza, timu zimeanza kuwasili nchini na kufanya vipimo vya afya na umri katika Taasisi ya Tiba na Mifupa Muhimbili (MOI). Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Katika taarifa iliyotolewa na shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF katika tovuti yao imesema utaratibu wa vipimo hivyo utaendelea leo katika taasisi hiyo kwa baadhi ya timu, huku timu ya Taifa ya Tanzania ‘Serengeti Boys’ imeshaanza kufanya vipimo hivyo jana na leo inaendelea na vipimo vingine.
Mashindano hayo yanatarajia kuanza Jumamosi tarehe 11 hadi 26 Agosti, 2018 kwenye Uwanja wa Taifa na Azam Complex, Chamazi Dar es Salaam.
Leave a comment