Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Tigo Fiesta yahairishwa
MichezoTangulizi

Tigo Fiesta yahairishwa

Spread the love

KAMATI ya Maandalizi ya Tamasha la Tigo Fiesta 2018 imesitisha tukio la kilele cha msimu wa tamasha hilo lililopaswa kufanyika leo tarehe 24 Novemba 2018. Anaripori Mwandishi Wetu … (endelea).

Tamasha hilo lilipaswa kufanyika kwenye viwanja vya Leaders vilivyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam, lakini kamati hiyo kupitia taarifa yake iliyotoa leo, imesema imesitisha kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake.

“Tunaomba radhi kwa madhara yoyote yatakayosababishwa na hili. Ambao walishanunua tiketi, kwa wale walionunua kupitia Tigo Pesa, fedha zao zitarejeshwa moja kwa moja kwenye simu zao kupitia mtandao, wlaionunua kwenye vituo vya mauzo wafike kwenye vituo wlaivyonunulia tiketi wakiwa na tiketi zao kwa ajili ya kurudishiwa fedha,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Kabla ya kamati hiyo kusitisha tamasha hilo, jana tarehe 23 Novemba 2018 Ofisi ya Afisa Utamaduni Manispaa ya Kinondoni ilitoa tamko la kusitisha kibali cha kufanyika tamasha hilo Leadres Club na kuhamishia katika uwanja wa uwanja wa Tanganyika Peackers ulioko Kawe.

Tamko hilo lilieleza kuwa, usitishaji huo unatokana na malalamiko ya baadhi ya wananchi na wagonjwa waliolazwa hospitalini kutokana na matangazo yanayoambatana na muziki unaopigwa kwa sauti kubwa katika tamasha hilo,na kuhatarisha afya za wagonjwa ikiwemo wa moyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

error: Content is protected !!