Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo TFF yapangua tena ratiba ya Ligi Kuu Bara
Michezo

TFF yapangua tena ratiba ya Ligi Kuu Bara

Spread the love

MICHEZO namba 14 na 19 ya Ligi Kuu Bara kati ya mabingwa watetezi Simba na Mbeya City na ule wa Azam FC dhidi ya Ndanda itachezwa siku ya Jumatatu 27 Agosti, 2018 badala ya 25 Agosti, 2018 kama ilivyopangwa hapo awali kutokana na mabadiliko yaliyofanywa na bodi ya ligi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Katika sehemu ya barua iliyotoka bodi ya ligi iliyosainiwa na Mwenyekiti wake Boniface Wambura imeonesha sababu za kusogeza michezo hiyo mbele ni kupisha maandalizi ya mchezo wa fainali wa kombe la CECAFA U-17.

“Mabadiliko haya yametokana na Uwanja wa Taifa kufanyika maandalizi kwa mchezo wa fainali za CECAFA U-17 ambao utachezwa tarehe 26.08.2018 (Jumapili)”

Hii ni mara ya pili kwa bodi ya ligi kupangua michezo ya Ligi Kuu kwa msimu huu wa 2018/19 kutokana na sababu za kuingiliana kwa shughuli za matumizi ya viwanja na hali hiyo inatokea kutokana na 90% ya klabu zinazoshiliki ligi hiyo havina viwanja vyao binafsi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!